0 0
Read Time:1 Minute, 0 Second

WU® MediaPRODUCTION LIMITED

Generali Venance Salvatory Mabeyo Mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Leo jumamosi tarehe 28/05/2022 ametembelea Ubalozi wa Tanzania mjini Rome Italy na kusaini kitabu Cha wageni.

Mkuu wa Majeshi amekutana na kuzungumza na wafanyakazi na maafisa wa Ubalozi wa Tanzania mjini Rome Italy.

Mkuu wa majeshi yupo kwenye ziara fupi ya kikazi nchini Italia.

General Mabeyo ni mkuu wa majeshi wa nane kuteuliwa,aliteuliwa nafasi hiyo tarehe 6 February 2017 na aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania awamu ya Tano Hayati Dr John Pombe Magufuli.

Mkuu wa Majeshi (CDF) General Mabeyo akisaini kitabu Cha wageni
General Mabeyo akisaini kitabu Cha wageni kwenye Ubalozi wa Tanzania mjini Rome Italy
Kulia mwenye koti nyeusi ni HOC Madam Jubilata Shao akiongea na General Mabeyo
Mkuu wa utawala wa Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mjini Rome Italy, HOC Madam Jubilata Shao akimkabidhi kitabu Cha wageni Mkuu wa majeshi mara alipotembelea ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Italy Leo jumamosi terehe 28/05/2022.
Madam Jubilata akimpokea mkuu wa majeshi General Mabeyo.

Picha kwa hisani ya:

Andrew C.Mhela

WU® MEDIA (ROME)

Happy
Happy
0 %
Sad
Sad
0 %
Excited
Excited
0 %
Sleepy
Sleepy
0 %
Angry
Angry
0 %
Surprise
Surprise
0 %