
WU® MediaPRODUCTION LIMITED
“NI KAMA HAZUILIKI TENA MWAKA 2025.”
George Michael Uledi.
Kyela,Mbeya.
August 8,2022.

Mizinga mitatu mikubwa ya kivita kwa maana ya makombora ya masafa yaani “artillery” iliyopigwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Taifa,Mh.Mama Samia Suluhu Hassan tokea mipaka ya Kasumulu wilayani Kyela kuelekea maeneo ya wilaya ya Mbalali, imetosha kabisa kufagia na kusambaratisha ndoto,chokochoko na tamaa zote za adui yaani “CDM”katika kutamani majimbo ya Mkoani Mbeya kuelekea mwaka wa uchaguzi 2025!
Wakati huu CDM wakijinasibu angalau kutaka kurudi mjengoni Dodoma Mwaka 2025 na hasa tageti yao kubwa kwa sasa ikiwa kurudisha majimbo ya Mbeya Mjini,Momba na Iringa Mjini ambapo kwa sasa wameamua kuweka Kambi ukanda wa nyanda za Juu Kusini,ni kama tayari wamepigwa “ambush” mapema kabisa!
Mama Samia, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, alimua kimkakati kudeploy silaha zake kwanza katika Jiji la Mbeya na na baadae kuanza kumshambulia adui zake akitokea Jiji la Mbeya kuelekea wilayani Chunya,wilayani Kyela na baade akaamua kuwithdraw vikosi vyake maeneo ya Mbalali,akijipanga tena kwa ajili ya kuiteka Njombe leo jioni!
Akiwa Wilayani Chunya,Mkoani Mbeya,Mwenyekiti huyo wa CCM Taifa huku akiongozana na Katibu Mkuu wake wa Chama,Comred Daniel Chongoro, huku mkononi wakibeba ajenda kuu mbili ambazo Serikali ya CCM imezitekeleza kwa ufanisi mkubwa, moja(i)ikiwa ajenda ya Maji na pili (ii)ikiwa ni ajenda ya kutaka kuufungua Mkoa wa Mbeya kwenda Mikoa ya Tabora,Singida na hata Katavi baada ya kuzindua Barabara ya Mbeya-Singida -Tabora kwa kiwango cha lami”Mkeka”!
Akijibu Ilani ya uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020-2025 ambayo moja kwa moja inagusa kwa asilimia 100% Mkoa wa Mbeya,Comred Chongolo alisema, Serikali imetenga karibia Trilioni moja kwa maana ya Bilioni 900+ kwa ajili ya sekta ya kilimo na hasa kilimo cha kisasa cha umwagiliaji ambapo wilaya kama ya Mbalali kupitia miradi yake mikubwa ya umwagiliaji ya Kapunga inaguswa moja kwa moja!
Kana kwamba Mwenyekiti na Katibu wake wa CCM, walikuwa na nia moja ya wazi kabisa ya kutaka kuisambaratisha chakali ngome ya CDM Mkoani Mbeya,pia Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh Tulia Ackson Mwansasu nae akapigilia msumari wa moto ndani ya kidonda cha CDM kwa kuomba barabara za lami za mitaa yote katika Jiji la Mbeya!Imeisha hiyo!
Ujenzi wa barabara “Mkeka” ya lami ya njia nne kutoka mji wa Igawa mpaka boda ya wajanja TUNDUMA Mkoani Songwe karibia Kilometa 250, ndio kabisa imeenda kuinyamazisha ngome ya CDM katika Mkoa wa Songwe na Mkoa wa Mbeya!Kwa kifupi ni kwamba CDM inakufa kutokana na utekelezaji mzuri wa ahadi kwenye Ilani ya uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020-2025!
Kana kwamba Mama yangu Samia Suluhu Hassan, ameamua kuisambaratisha CDM ukanda wa nyanda za Juu Kusini,leo jioni ataelekeza silaha zake za kivita”artillery” uelekeo wa Mkoa wa Njombe kwa Afande Mstaafu, Antony Mtaka,Mkuu mpya wa Mkoa wa Songwe!
Ziara hiyo ya kihistoria ambayo iliambatana na uwepo wa wakuu wa maeneo yote ya Jeshi lake ndani ya CCM kwa maana ya Wakuu wa Kamandi,Bataliani pamoja na Vikosi vyote vya Chama cha Mapinduzi,chini ya Mnadhimu Mkuu wa CCM,Comred Daniel Chongolo!Pembeni ya Amiri Jeshi Mkuu, alikuwepo Mkuu wa Mhimili wa Bunge, PhD Tulia Ackson Mwansasu!
Mpango huu wa kivita wa CCM”Sand Model” ambao inaonekana umechorwa timamu kabisa na Kanali Mstaafu wa JWTZ ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM na Political Magician,Afande wetu Kanali, Abdullaman Kinana!Wiki Jana,Kanali Kinana akiongozana mbeba Itikadi ya Chama cha Mapinduzi, Comred Shaka Hamdu Shaka, waliweza kusafiri na kwenda kumkagua na kuchunguza adui”recce” kabla ya kuamua kuingiza vikosi rasmi katika uwanja wa medani kupitia kwa Mh.Rais Samia katika Mikoa ya Katavi,Songwe na Mbeya!
Kwangu hii ni moja ya ziara kubwa na bora zaidi kwa CCM labda tangu Mama yangu Samia Suluhu Hassan aingie madarakani na imempa vipimo sahihi vikubwa vitatu kuhusu itimamu wake (i)kukubalika kwa mipango na sera zake,(ii)kukubalika kwa Serikali yake na(iii)tatu ni ufanisi katika utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020-2025 yaani ” To Measure her Political Indurance”!
20255555???,Acha CCM Iendeleee!
+255746726484.







