
Mheshimiwa Balozi Mbundi, tarehe 15 Januari, 2021, aliongoza majadiliano baina ya Poland na Tanzania.
Mjadiliano hayo yaliyolenga kuimarisha ushirikiano hususan katika masuala ya biashara na uwekezaji. Kwa upande wa Tanzania washiriki walikuwa ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Kilimo; Mjumbe kutoka Wizara ya Fedha na Mipango; Watendaji wa NFRA; na Watendaji wa TBA.Kwa upande wa Poland, walioshiriki ni pamoja na Mheshimiwa Krzysztof Buzalski Balozi wa Poland nchini Tanzania na Wawakilishi wa makampuni kutoka Poland ya Feerum S.A na Unia Spzo.o.