0 0
Read Time:1 Minute, 28 Second

Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi amesema nguvu inayotumika kupambana na wabadhirifu wa mali za umma visiwani humo si nguvu ya soda na mapambano hayo ndio kwanza yameanza.

Kadhalika, amesema wizi, ubadhirifu wa mali za umma ni mambo aliyoyavalia njuga na hataki masihara na kusisitiza kuwa ataendelea kuondoa muhali ili wale wote wanaohusika au waliohusika kwenye ubadhirifu wachukuliwe hatua.

Dk Mwinyi aliyasema hayo Ikulu mjini Zanzibar wakati akizungumza na wahariri na waandishi wa vyombo vya habari Tanzania kuhusu siku zake 100 madarakani.

Happy
Happy
0 %
Sad
Sad
0 %
Excited
Excited
0 %
Sleepy
Sleepy
0 %
Angry
Angry
0 %
Surprise
Surprise
0 %