
Singapore
Balozi wa Tanzania nchini Singapore mwenye makazi yake nchini Indonesia, Mhe. Macocha Tembele amewasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Singapore, Mhe. Tharman Shanmugaratnam katika hafla iliyofanyika Ikulu ya Istana Septemba 2025.
Katika mazungumzo yao, wawili hao waligusia masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Singapore katika sekta za biashara, uwekezaji, nishati na elimu.
