0 0
Read Time:37 Second

WU® MEDIA

Columbus Ohio

Watanzania Wamekusanyika kwa Sala (Misa) na Maombi Pamoja na kutoa salaam zao za mwisho kwa Msanii wa muziki wa Bongo Fleva na mwanaharakati wa kutetea haki za watu wenye ulemavu wa ngozi, Babu Sikare maarufu kama Albino Fulani aliyefariki siku ya tarehe 8/02/2023 kama taarifa zilivyopatikana kwenye mitandao

Albino Fulani ambaye amewahi kutamba na nyimbo kadhaa ikiwemo “Nafasi” aliyoshirikiana na Mwana FA, Sugu na Belle 9 amefariki Dunia akiwa Nchini Marekani.

Mipango ya Mazishi inaendelea na yanatarajiwa kufanyika nchini Tanzania mara baada ya taratibu za kusafirisha mwili kukamilika.

Mungu Amrehemu .. Amen

Watanzania wakijifariji Majonzi baada ya Sala na Maombi kwa marehemu Albino Flani aliyefariki siku ya tarehe 8/02/2023
Msanii Albino Flani



Happy
Happy
0 %
Sad
Sad
0 %
Excited
Excited
0 %
Sleepy
Sleepy
0 %
Angry
Angry
0 %
Surprise
Surprise
0 %