Read Time:34 Second
Jumuiya ya watanzania ugiriki ilisherehekea miaka 48 ya mapinduzi ya Zanzibar kwenye ofisi ya jumuiya J’mosi 14/02.Tulilazimika kuichelewesha kwa siku mbili kutokana na mihangaiko ya kikazi.
WABONGO UGHAIBUNI
Sherehe zilianza kwa wimbo wa Taifa na kufuatiwa na risala fupi ya Mwenyekiti mwanzilishi wa Jumuiya yetu bw.Suleiman Nassib (DIDOS)ambae alisisitizia umuhimu wa umoja na ushirikiano.
Ilifuatiwa na shukurani za bi.Joan mwakilishi wa kikundi cha wanafunzi wa Holland tuliowakaribisha rasmi katika sherehe yetu.
Baadae mke wa Mwenyekiti Bi Asha Chunda alikata keki maalum ya mapinduzi na bw.Jackson na bi Sandra walitumbuiza na kuchangamsha ukumbi kwa nyimbo zao zilizowanyanyua hata wageni wetu.
Sherehe ziliendelea hadi alfajiri
KAYU LIGOPORA
KATIBU WA JUMUIYA YA WATANZANIA UGIRIKI
Paris France WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema kuna haja ya kutafuta mbinu mpya ya kukieneza Kiswahili baada ya kuwa kimepata hadhi ya kimataifa. “Kadiri Kiswahili kinavyoendelea kupata hadhi ya…
Moscow, Urusi RAIS Dkt. Samia Suluhu Hassan amesifu mchango wa Chuo Kikuu cha Urafiki cha Watu wa Urusi (RUDN) katika ukombozi wa nchi za Afrika akisema kimesadifu maono ya viongozi…

















