Read Time:34 Second
Jumuiya ya watanzania ugiriki ilisherehekea miaka 48 ya mapinduzi ya Zanzibar kwenye ofisi ya jumuiya J’mosi 14/02.Tulilazimika kuichelewesha kwa siku mbili kutokana na mihangaiko ya kikazi.
WABONGO UGHAIBUNI
Sherehe zilianza kwa wimbo wa Taifa na kufuatiwa na risala fupi ya Mwenyekiti mwanzilishi wa Jumuiya yetu bw.Suleiman Nassib (DIDOS)ambae alisisitizia umuhimu wa umoja na ushirikiano.
Ilifuatiwa na shukurani za bi.Joan mwakilishi wa kikundi cha wanafunzi wa Holland tuliowakaribisha rasmi katika sherehe yetu.
Baadae mke wa Mwenyekiti Bi Asha Chunda alikata keki maalum ya mapinduzi na bw.Jackson na bi Sandra walitumbuiza na kuchangamsha ukumbi kwa nyimbo zao zilizowanyanyua hata wageni wetu.
Sherehe ziliendelea hadi alfajiri
KAYU LIGOPORA
KATIBU WA JUMUIYA YA WATANZANIA UGIRIKI
Leo ni siku ya kihistoria kwa Taifa letu. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amezindua rasmi Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Julius Nyerere (JNHPP)…
Zanzibar Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) zimekubaliana kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kijamii katika maeneo ya kimkakati ikiwemo biashara na uwekezaji, kilimo, madini, nishati, usafirishaji, miundombinu, afya…

















