1 0
Read Time:1 Minute, 17 Second

ITALY – ZANZIBAR BUSINESS AND INVESTIMENT FORUM

Na Mwandishi wetu

Zanzibar

WU Media PRODUCTION LIMITED

Kongamano kubwa la kibiashara Kati ya Italy na Tanzania limefanyika Leo Zanzibar ikiwa ni sehemu ya kwanza ambapo itafuatiwa na kongamano la pili litakalofanyika siku ya kesho Jijini Dar Es Salaam.

Kongamano hilo ambalo lililofunguliwa na Makamu wa kwanza wa Rais Mh. Othman Masoud  ambae alimuwakilisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dr Hussein Mwinyi, limemalizika kwa mafanikio makubwa.

Balozi wa Tanzania nchini Italy Mh Mahamoud Thabit Kombo na Balozi wa Italy nchini Tanzania Mh Marco Lombardi, walipata fursa ya kuongea na wadau wa biashara wa Italy na Tanzania. Katika kuhimiza Diplomasia ya Uchumi, Balozi wa Tanzania nchini Italy Mh Mahamoud Thabit Kombo aliwataka wadau wa biashara wa Tanzania kuchangamkia fursa za kibiashara hasa za masoko ya bidhaa za KILIMO kama Parachichi nk.

Mgeni rasmi katika kongamano kubwa la kibiashara Mh. Othman Masoud  Makamu wa kwanza wa rais wa Zanzibar wakati akifungua rasmi Kongamano.
Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Mahmoud Thabi Kombo akiongea na wafanya biashara wa Italy na Tanzania katika forum iliyofanyika leo Zanzibar
Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Mh. alimuwakilisha Rais Mwinyi katika kongamano hilo kubwa la kibiashara liliofanyika Zanzibar leo jumatano 28/09/2022
Diapora kutoka Italy pia wamehudhuria kongamano la biashara
Mh Mahamoud Thabit Kombo Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Italy akiongea na wadau wa biashara wa Italy na Tanzania wakati wa kongamano la biashara lilofanyika Zanzibar 28/09/2022
Happy
Happy
50 %
Sad
Sad
0 %
Excited
Excited
50 %
Sleepy
Sleepy
0 %
Angry
Angry
0 %
Surprise
Surprise
0 %