05.11.2022
Balozi Asha-Rose Migiro amezindua mgahawa wa kwanza jijini Edinburgh, Scotland, utakaopika chakula cha Kitanzania.
Balozi wa Jamhuri ya Tanzania nchini Uingereza Dr Asha-Rose Migiro amewapongeza Margaret Mazoeleka na familia yake kwa hatua kubwa na kusema kuwa mgahawa huu Utakidhi mahitaji ya wadau na kuitangaza Tanzania.
Diaspora wana nafasi kubwa ya kutangaza nchi ya Tanzania kwenye nyanja mbalimbali ikiwemo Mila na Utamaduni wa Mtanzania.