1 0
Read Time:1 Minute, 13 Second

Shula’s kitchen

Na Mwandishi wetu

Antwerpen Belgium 28/01/2023

Ubalozi wa Tanzania nchini Ubelgiji ukiwakilishwa na ndugu Anthony S.Mtafya (HOC) ambae pia ameongozana na Bi Vivian A.Rutaihwa na Ndugu Juma Salum ambae ni msimamizi wa dawati la diaspora Ubalozi wa Tanzania Belgium. wamehudhuria sherehe ya ufunguzi wa Restaurant ya Mtanzania (DIASPORA) anaeishi mjini Antwerpen

Katika ghafla hiyo pia ilikuwa na bahati ya pekee kuhudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Italy Mh Mahamoud Thabit Kombo alieongozana na Mkewe.

Katika hafla hiyo walishiriki Wana diaspora kutoka nchini Belgium na Luxembourg ambako pia ni eneo la uwakilishi wa ubalozi wa Tanzania Belgium

Mwenyekiti wa Diaspora nchini Ubelgiji Ndugu Riziki Thomas wakati akiongea na WABONGO UGHAIBUNI MEDIA kwa njia ya mtandao alisema “Ubalozi wa Tanzania nchini Belgium pamoja na majukumu makubwa ya uwakilishi wa Nchi yetu lakini wamekuwa karibu na Diaspora kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Jumuiya ya Watanzania kuwaunganisha Watanzania, kushirikiana katika kuleta Maendeleo kwa Watanzania nchini Belgium ili waweze kuzitumia fursa za uwekezaji nyumbani Tanzania, na kwa kufanya hivyo kutaweza kuchangia Maendeleo.

Shula’s kitchen ni restaurant ambayo itawafanya Watanzania na watu wa East Africa kujisikia wako nyumbani kwani Dada Ashura ni mbobezi wa mahanjumati.

Mwakilishi wa Balozi Ndugu Anthony S. Mtafya akiongea kwenye ufunguzi Rasmi wa Shula’s kitchen mjini Antwerpen Belgium.
Picha ya Pamoja
Katika picha Ashura akiwa na Mama yake na Mumewe
WU®
Mwenyekiti wa Diaspora Belgium na Luxembourg Ndugu Riziki Thomas

Picha na Lilian Nabora

Antwerpen Belgium

#Equitydiasporabanking
Happy
Happy
67 %
Sad
Sad
0 %
Excited
Excited
33 %
Sleepy
Sleepy
0 %
Angry
Angry
0 %
Surprise
Surprise
0 %