Na Mwana Habari wetu A.BOI , Durban
WU® MEDIA
Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Afrika ya Kusini Mh. Gaudence Milanzi anakutana na Watanzania wanaoishi jijini Durban muda huu.
Watanzania hao ambao wako chini ya mwamvuli wa Jumuiya ya Watanzania Durban wamejumuika kwa wingi kwa ajili ya kumsikiliza mlezi wa Diaspora ambae ni Mh Balozi lakini pia kuja kufanya shughuli maalumu zinazohusu mustakabali wa Jumuiya Yao kwa ujumla.
![](https://www.tzabroad.com/wp-content/uploads/2023/02/IMG-20230218-WA0214-976x1024.jpg)
Mkutano huo unahusu kutambulishwa rasmi kwa Balozi Jumuiya ya Watanzania Durban Natal. Pamoja na utambulisho huo pia lipo zoezi la utoaji kadi kwa wanachama wa Jumuiya ya Watanzania Durban. Sambamba na kadi pia uongozi utatoa muhtasari wa mwenendo wa Chama kwa ujumla.
Mwanahari wetu Bado yupo sehemu ya tukio hivyo kwa Habari zaidi TEMBELEA mtandao wako huu wa Wabongo Ughaibuni Media Production Limited.