
Na Mpiga picha wetu Michael Davide
Rome Italy

Marehemu Hamisi Mpini
Watanzania nchini Italy Leo ijumaa tarehe 12/05/2023 wamekutana Rome kumsindikiza Marehemu Hamisi Suwedi Mpini aliyefariki tangu tarehe 16/04/2023 wakati akiwa hospitalini akipatiwa matibabu.

Katika mazishi hayo yaliyoongozwa na Jumuiya ya Watanzania Rome chini ya mwenyekiti wake Ndugu Leonce Uwandameno, Mwenyekiti alitoa shukran kwa Watanzania kwa kujitokeza na wote ambao wamechangia msiba kwa njia moja ama nyingine.
Ubalozi wa Tanzania uliwakilishwa na Mh. Sigfred Nnembuka ambae pia aliambatana na muambata wa Kilimo na mhasibu wa Ubalozi.
Jumuiya ya Watanzania Italia in CAMPANIA iliwakilishwa na Katibu wa Jumuiya Dada Cecilia Lemmah.











