
Viena Austria
Watanzania nchini Austria Wamekusanyika kwa ibada na Sala kumuaga na kumuombea pumziko la milele aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Austria Mh Celestine Mushi.
Hayati Balozi Mushi amekutwa na umauti kwa ajali ya gari alipokuwa njiani kuelekea Moshi kuungana na familia yake kwa mapumziko ya sherehe za Krismasi.
Wanadiplomasia wa Tanzania wamekuwa na Wakati mgumu Sana kwa msiba wa mwenzao maana ni hivi Karibuni tu walikuwa Pamoja katika vikao Kazi vilivyokuwa vikiendelea nchini Tanzania.
Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Italy, Mh Mahamoud Thabit Kombo aliandika katika ukurasa wake wa Instagram maneno mazito yenye kuashiria kuguswa kwa kiasi kikubwa kwa msiba wa Balozi Mushi. “


Nae Balozi Anisa Mbega aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram












