
WU® MediaPRODUCTION LIMITED
Taarifa kwa umma
Mhe. Humphrey Polepole Balozi wa Tanzania Nchini Malawi amekuwa na mazungumzo na Mhe. Andrew P.E.Z Kumwenda. Balozi wa Malawi Nchini.
Katika Mazungumzo hayo, Balozi Polepole amemhakikishia ushirikiano wa juu kwa masuala mbalimbali ikiwa ni sehemu ya kuendelea kukuza na kuimarisha mahusiano baina ya Tanzania na Malawi.
Pamoja na mambo mengine, Balozi Polepole amegusia fursa kubwa ya kutumia Ushoroba wa kusini (Mtwara Corridor) ili kuwezesha usafiri na usafirishaji wa bidhaa na huduma kwenda na kutoka Malawi.









