
Read Time:1 Minute, 18 Second
WU® MediaPRODUCTION LIMITED
Na Mwandishi wetu
Zanzibar










Akitoa Salamu za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Hemed ameeleza kuwa SMZ inathamini juhudi zinazofanywa na Taasisi Binfasi katika kuunga mkono Juhudi za Serikali katika kuwatumikia Wananchi wake.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ameeleza kuwa Juhudi zinazofanywa na Taasisi ya Mwanamke Initiatives Foundation ni za kupigiwa Mfano hasa kuunga mkono katika Sekta ya Elimu Nchini akitolea Mfano kufadhili vifaa kwa Skuli na Kambi za Wanafunzi wa Kidato cha Nne Mkoa wa Kusini Unguja katika kukuza ufaulu kwa Mkoa huo.
Aidha ameeleza kuwa miongozo ya Viongozi wakuu wa Nchi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan pamoja na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt Hussein Ali Mwinyi imesaidia kurahisisha ufanyaji kazi wa Taasisi Binafsi kwa kuinua wigo kwa Taasisi nyengine.
Imetolewa na Kitengo cha Habari (AMPR)
19 Juni 2022








