
WU® MEDIA
Balozi wa Tanzania nchini Italia Mh.
Mahmoud Thabit Kombo amewasilisha hati ya utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Malta, Dk. George Vella katika Ikulu ya Malta.
Baada ya kuwasilisha hati hizo za utambulisho kwa Mhe. Rais Vella, viongozi hao wawili walisisitiza zaidi kuimarishwa kwa ushirikiano katika nyanja mbalimbali za kiuchumi na kisiasa na kujitolea kwa Malta kuwa daraja kati ya Afrika na Umoja wa Ulaya.
Katika mazungumzo yao walisisitiza suala la kutengeneza fursa katika nyanja za elimu, utalii, utamaduni, uvuvi, meli, biashara na uwekezaji.

