
Maonesho yalianza 11-12-12-13 March, 2023


Tan Warriors Wasaini mikataba yenye fursa kubwa kwa Vijana wa TANZANIA
TAN WARRIORS SPORTS ACADEMY KUWA KITUO KIKUBWA CHA MICHEZO AFRIKA YA MASHARIKI
Tarehe 11-12-13 March 2023 Tanzania ilishiriki maonesho ya kimataifa ya biashara yaliyofanyika mji wa FERMO mkoani MARCHE nchini Italy. Katika maonesho hayo makubwa ushiriki wa Tanzania ukiongozwa na kuratibiwa vyema na Ubalozi wa Tanzania nchini Italy. Katika maonesho hayo ya kibiashara ambapo mwaka huu ilichaguliwa Tanzania kushiriki kama Nchi ya Afrika.



Pamoja na bidhaa mbalimbali za Tanzania kuoneshwa na kutangazwa katika maonesho hayo, pia Tanzania ilipewa nafasi ya kuonyesha mapishi ya chakula katika maonesho na pia kuweza kuandaa CHAKULA Rasmi Cha jioni ambapo walihudhuria viongozi mbalimbali akiwemo Mstahiki Meya wa FERMO akiambatana na viongozi na wananchi walioalikwa.
Katika HAFLA hiyo ya chakula Cha jioni Balozi wa Tanzania nchini Italy Mh Mahamoud Thabit Kombo alipata nafasi ya kuongea na wageni waalikwa, Mh Balozi alitoa shukran kwa Tanzania kupata nafasi hiyo adhimu kushiriki katika maonesho na kuitangaza Tanzania kibiashara, uwekezaji,Mila na utamaduni. Ushiriki wa Tanzania katika maonesho hayo umeleta matokeo chanya kwani Mh Balozi alialikwa na kutembelea Chuo Kikuu Cha CAMERINO.


Chuoni hapo alipokelewa na mkuu wa Chuo hicho Balozi Mahamoud Thabit Kombo akiwa kaongozana na Mkewe Pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Diaspora nchini Italy Ndugu Kagutta Maulidi, Dada Eva Nangela ambae ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania mji wa Genova Italy ambae pia ni Mratibu (coodinator) wa Tan Warrious Sports Academy, pia alikuwepo mjumbe wa Jumuiya ya Watanzania Napoli Ndugu Salim Awadh, baada ya mazungumzo mafupi mkuu wa Chuo na Mh Balozi walifanya ziara ya kutembelea majengo na vitengo mbalimbali vya Chuo hicho chenye historia kubwa tangu kianzishwe mwaka 1336.
Kwa umuhimu wa pekee katika ziara hiyo hapo chuoni Mh Balozi aliongozana na Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya Trinity Southern Sahara na Tan Warrious Sports Academy Ndugu Mainga Ole Kalaita aliye ambatana na Mkurugenzi wa ufundi wa Sports Academy hiyo Ndugu Suleiman Khalid Sharrif. Mapema siku hiyo Mkurugenzi Mtendaji huyo alisaini mikataba miwili mikubwa, mmoja ulikuwa ni wa ujenzi wa miundombinu ya Sports Academy ambayo itakuwa ya viwango vya kimataifa, pia Tan Warrious ilisaini mkataba na Chuo hicho kikuu Cha CAMERINO kushirikiana katika kutoa fursa za vijana wenye vipaji kushiriki katika mafunzo na elimu ya juu. TAN WARRIORS SPORTS ACADEMY ipo mjini MOROGORO inategemewa kuwa kituo kikubwa Africa ya mashariki kitakachokuza vipaji na kuchangia kwa kiasi kikubwa kwenye sekta ya michezo Tanzania.


Mh Balozi Mahamoud Thabit Kombo akiongozana na Diaspora Pamoja na Mkurugenzi wa Trinity Southern Sahara Ndugu Mainga Ole Kalaita walitembelea kiwanda kikubwa cha kuchakata Tumbaku na uzalishaji wa Sigara.














We are very grateful to the leadership of Tanzania, led by Mama Samia, the President of Tanzania, and Mr. Dr. Alkhasan Mwinyi, the President of Zanzibar, for being concerned about Tanzania and its economic development, so that it will be known later and that Tanzania is one of the best countries that has made great strides economically and development, an issue that took place in Italy. it is a big issue to take the next step in development.
Asante sana