
“TANZANIA IMEPATA MAFANIKIO MAKUBWA
WU® MediaPRODUCTION LIMITED
Maonyesho ya kimataifa ya kilimo MacFrut 2022 yamemalizika Jana kwa mafanikio makubwa. Ujumbe wa Tanzania uliongozwa na Balozi wa Tanzania nchini Italy Mh. Mahamoud Thabit Kombo Pamoja ulijumuisha wizara ya kilimo na wadau wa mbalimbali ambao walifika Rimini Italy kushiriki kwenye haya Maonyesho ya kimataifa.
Wakati akiongea na Wabongo ughaibuni Media katika kuhitimisha Mh Balozi ameeleza kwa kirefu Kuhusu Changamoto Pamoja na mafanikio makubwa yaliyopatikana kwenye maonesho haya. Sambamba na kutoa maoni yake Mh.Balozi pia amewatangazia Watanzania kujiandaa kwa maonesho ya mwakani 2023 ambayo tunahitaji maandalizi makubwa zaidi.
Katika maonesho haya Mh Balozi pia alipata nafasi ya kukutana na wadau mbalimbali ambao wameonesha Nia kubwa ya kuwekeza Hasa kwenye sekta ya kilimo Cha matunda na mbogamboga.
























