

Mkimbiaji wa mbio ndefu katika mashindano ya Olympic nchini Japan anayeiwakilisha Tanzania mwaka huu Alphonce Felix Simbu ameingia katika kumi bora.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo nchini, Yusuph Singo Omary, Simbu ameshika nafasi ya SABA katika mbio za Marathoni zilizomalizika leo.
Omary amesema kwenye mashindano ya Olympic ya mwaka huu mbali na mkimbiaji Simbu, Tanzania iliwakilishwa pia wakimbiaji Gabriel Geay na Failuna Matanga ambao hawakuingia kumi bora.









